February 24, 2011

JIHADHARINI NA HII Kanyaboya aka "SCAM"

Hi, My name is Barbara Backlund. I am on a volunteer job working with Global Youth Development and Peace Initiative (GYDPI), Seattle, WA, USA. We are cordially inviting you to our twin combined conference (GYDPI 2011) to be held in Vancouver - Canada from April. 18th - 21th, 2011 and Athens - Greece from April. 25th - 29th, 2011. which is organized in conjunction with Greece board for tourism.
If you are interested to participate and want to represent your country, you should contact the conference organizers below for details and participation Information. You are invited by Mrs Barbara Backlund and your invitation number is 116.
The benevolent donors of the Organizing Committee will provide round trip Air tickets and accommodation for the period of participants Stay in Vancouver - Canada, to all invited/registered participants. You will only be responsible for your hotel booking in Athens - Greece where the second phase of the conferences will be held. To be registered, participants must be ready to attend both conferences as the second is a continuation.
If you are a holder of an international passport that may require visa to enter Canada / Greece the organizing committee is responsible for all visa arrangements within the time frame and travel assistance.
You can Contact the Conference secretariat with the address below for detailed information. By Tel: +1 206-333-0338 By Fax: +1 206-984-3466 Email: dupeters@eml.cc
Contact them with your full names, address and country. I look forward to meeting you at the conference. Sincerely, Barbara Backlund. deposit@atefund.com
Nimepata leo email hii baada ya ku -Google nikakuta jamaa wameanza siku nyingi hawa cheki HAPA

February 22, 2011

Mkurugenzi Manispaa Zanzibar amwagiwa tindikali

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimfariji Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa Zanzibar Rashid Ali Juma (45) alipomtembelea leo katika Hospitali ya Aga khan jijini Dar es salaam alikolazwa kwa matibabu kutokana na kuumia vibaya sehemu za usoni, tumboni, kifuani na ubavuni baada ya kumwagiwa Tindikali na Mtu asiyejulikana, wakati alipokuwa amekaa nje ya Msikiti wa Amani mjini Zanzibar baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Insha saa 2:45 usuku, siku ya Alkhamis . Kwa muujibu wa madaktari wanaomhudumia Mkurugenzi huyo, wamemuambia Makamu wa Rais kuwa hali yake inaendelea Vizuri.

©VPO.

February 21, 2011

Mmiliki wa Dowans akataa kukutana na Ngeleja na kupigwa picha

WAKATI Mjadala wa Dowans ukibaki kwenye swali la nani mmiliki wake, raia wa Oman, Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi amejitokeza na kukiri kuimiliki kampuni hiyo inayoidai Tanzania mabilioni ya shilingi. Al Adawi alikutana na wahariri wa vyombo vya habari nchini jana na kueleza ujio wake kuwa umelenga kukutana na Tanesco na kujadili suala la malipo ya Sh94 bilioni ambayo kampuni yake inaidai Tanzania.

Ujio wa Al Adawi umemaliza mjadala uliogubika umiliki wa Dowans na kuwachanganya Watanzania huku baadhi yao wakiamini kuwa kampuni hiyo inamilikiwa na mfanyabiashara maarufu nchini, Rostam Aziz. Al Adawi ni mmoja wa watu ambao majina yao yako kwa Wakala wa Usajili wa Kampuni nchini (Brela) waliojiandikisha kama wamiliki wa kampuni hiyo ya Dowans.

Watu wengine waliotajwa na Brela kuwa ni wamiliki wa Dowans Tanzania Ltd, ambao ni Dowans Holding S.A, Costa Rica na Portek Systems and Equipment (PTE) Ltd na uraia wao kwenye mabano ni Andrew James Tice na Guy Picard (Canada), Gopalakrishnan Balachandaran (India), Stanley Munai (Kenya) na Hon Sung Woo (Singapore).

Akizungumza katika mkutano huo huku akigoma kupigwa picha, Al Adawi alisema yuko tayari kuzungumza na Tanesco kuhusu fidia ya Sh94 bilioni (hakutaja kiasi), baada ya kuvunjwa kwa mkataba baina ya kampuni yake hiyo na Tanesco.

"Nimekuja kwa mambo mawili; moja ni kuondoa sintofahamu iliyopo hivi sasa kuhusu kampuni ya Dowans na kuangalia kama kuna uwezekano wa kuwapo suluhisho la kile kilichopo hivi sasa kuhusu Dowans," alisema Al Adawi. Kwa mujibu wa mfanyabiashara huyo, ambaye ni Mwanajeshi aliyestaafu katika ngazi ya Brigedia Jenerali, Tanzania ni nchi inayovutia kibiashara na inayofuata sheria za uwekezaji.

Source: Mwananchi

February 18, 2011

Amiri Jeshi Mkuu alipongeza Jeshi

TAARIFA MAALUM KUHUSU MAAFA YA GONGOLAMBOTO

Ndugu Wananchi,

Kama mjuavyo, jana usiku jiji la Dar es Salaam lilipata mtikisiko mkubwa kutokana na milipuko ya mabomu iliyokuwa inatokea katika ghala kuu la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lililoko Gongolamboto katika viunga vya Dar es Salaam.

Milipuko hiyo imesababisha maghala 23 kuteketea kabisa na majengo kadhaa ya shughuli mbalimbali hapo kikosini kuharibika kwa viwango mbalimbali. Mabweni mawili ya kuishi wanajeshi nayo yaliteketea. Aidha, risasi nyingi, mabomu mengi, silaha na magari kadhaa nayo yameharibiwa na mengine kuteketea. Jeshi letu na nchi yetu imepata hasara kubwa sana.

Katika maafa haya makubwa kwa taifa letu, raia nao wameathirika kwa namna mbalimbali. Nyumba kadhaa za kuishi na majengo ya huduma za jamii nayo yameharibiwa na mabomu yaliyoangukia humo. Zipo ambazo zimeungua kabisa na zipo zilizopata uharibifu mkubwa na zipo zilizopata uharibifu wa viwango vya chini.

Lakini baya zaidi, katika mlipuko huo, ndugu zetu 20 wamepoteza maisha na wengine zaidi wamejeruhiwa kwa aina na viwango mbalimbali. Baadhi yao walifika katika hospitali za Amana, Temeke na Muhimbili na kupatiwa matibabu. Wengine wameruhusiwa na wengine wapatao 135 bado wamelazwa. Idadi kamili hupanda na kushuka kutegemea na kupokelewa na kuruhusiwa kwa majeruhi.

Ndugu Wananchi,

Hakika taifa limepata hasara kubwa kwa ndugu zetu kufariki na kujeruhiwa. Napenda kutumia nafasi hii kwa uchungu mkubwa kuelezea masikitiko yangu na taifa kwa ndugu zetu waliopoteza maisha wakati ambapo taifa lilikuwa bado linauhitaji sana mchango wao.

Naomba ndugu wa marehemu wapokee mkono wa rambirambi kutoka kwangu na kupitia kwangu kutoka kwa Watanzania wenzetu wote. Tuwaombee kwa Mwenyezi Mungu marehemu wetu wapate mapumziko mema. Amin.

Aidha, kwa niaba yangu na ya Watanzania wenzangu wote, nawapa pole nyingi ndugu zetu wote waliojeruhiwa na kupata mshituko kutokana na milipuko ya mabomu iliyotokea jana usiku. Tunazidi kuwaombea wapone upesi ili waendelee na kazi zao za kujenga taifa pamoja na kujiletea maendeleo yao binafsi.

Leo asubuhi na baadae mchana nilitembelea eneo la tukio kule Gongolamboto na kuwatembelea wagonjwa katika hospitali za Amana, Temeke na Muhimbili. Nimeona madhara na hasara tuliyoipata pale Gongolamboto. Nimewaona na kuwafariji wagonjwa wetu. Nimezungumza na madaktari na wauguzi katika hospitali hizo. Nimewashukuru na kuwapongeza kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya usiku kucha ya kuwahudumia na kuokoa maisha ya ndugu zetu hao. Nimewatia moyo na kuwataka waendelee kuwahudumia vyema.

Ndugu Wananchi,

Napenda pia kutumia nafasi hii kuwapongeza viongozi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na wa Bohari Kuu ya Madawa kwa kuhakikisha kuwa dawa na vifaa vya tiba vinapatikana kwa urahisi na kwa wakati, Hali hiyo ndiyo iliyosaidia kuokoa maisha na kuwapunguzia machugu ndugu zetu waliojeruhiwa.

Baraza la Usalama

Ndugu Wananchi,

Leo alasiri mpaka usiku huu, tulikuwa na mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Taifa. Hiki ndicho chombo cha juu cha kumshauri Rais kuhusu masuala yahusuyo usalama wa taifa letu. Kwa uzito na unyeti wa tukio, niliamua kuitisha mkutano wa Baraza hilo mara baada ya maafa hayo kutokea.

Katika mkutano wetu, tumelitafakari kwa kina tukio hili na mambo mbalimbali yanayotokana na kuhusiana nalo. Baraza limeazimia kama ifuatavyo:

1. Tumesikitishwa sana na tukio hili na hasa vifo vilivyotokea na majeraha yaliyowapata ndugu zetu wengi. Baraza limetoa rambirambi kwa ndugu na jamaa wa marehemu. Aidha, tunawapa pole wale wote waliojeruhiwa na kuwaombea kwa Mola wapone upesi.

2. Kuhusu waliopoteza maisha, tumeamua kuwa, Serikali igharamie mazishi ya marehemu wetu hao popote ndugu watakapoamua wakazikwe. Baadae ndugu wa marehemu wapewe kifuta machozi.

3. Kuhusu waliojeruhiwa tumeamua kuwa Serikali igharamie matibabu yao. Baadae watakapotoka hospitali walipwe kifuta machozi kwa ulemavu walioupata.

4. Kamati ya Maafa ya Mkoa imeagizwa kushirikiana na Kitengo cha Maafa cha Taifa kilichopo Ofisi ya Waziri Mkuu kuwahudumia wananchi waliopoteza makazi yao au waliolazimika kuyakimbia makazi yao kwa nia ya kuokoa maisha yao. Ihakikishwe kuwa kwa haraka wanapatiwa makazi ya muda pamoja na huduma za malazi, chakula, maji, afya na usafi wa mazingira.

5. Aidha, Kamati ya Maafa ya Mkoa imeelekezwa kutengeneza taratibu nzuri zitakazohakikisha kuwa mapema iwezekanavyo, wananchi hao wanarejea makwao ili waendelee na shughuli zao za kawaida hasa sasa ambapo hatari ya milipuko katika maghala ya Gongolamboto haipo tena.

6. Baraza la Usalama limelipongeza Jeshi la Ulinzi kwa uamuzi wake wa haraka wa kuwatuma wahandisi wa medani kufanya kazi ya kutafuta, kutambua na kuyakusanya mabomu yote yaliyoangukia katika maeneo ya raia kwa nia ya baadae kuyaharibu.

7. Tunawaomba wananchi watoe ushirikiano wa hali ya juu kwa Jeshi kwa kuwapa taarifa wanapoyaona mabomu katika maeneo yo yote. Na, jambo kubwa zaidi tunawakumbusha wananchi kutii maelekezo ya Jeshi ya kutokuyagusa au kuchezea mabomu au hata vipande vipande vya mabomu vilivyodondoka katika maeneo yao.

8. Baraza la Usalama la Taifa, limeagiza Kamati ya Maafa ya Mkoa wa Dar es Salaam na Kitengo cha Maafa cha Taifa wazitambue mapema iwezekanavyo nyumba zilizoharibiwa, wenye nyumba na kuhakikisha kuwa matayarisho husika yanafanyika ikiwa ni pamoja na uthamini ili walipwe fidia wanayostahili bila kuchelewa.

9. Vile vile Kamati ya Maafa ya Mkoa imeagizwa kufanya yafuatayo:

(a) Kushirikiana na Jeshi la Polisi kuwatafuta watoto waliopotea na kuwaunganisha na familia zao.

(b) Kuongoza, kuratibu na kusimamia utekelezaji wa masuala yote yahusuyo waliofariki, waliojeruhiwa na waliohama makazi yao, na huduma zao stahiki.

10. Baraza la Usalama limetoa pole nyingi kwa Mkuu wa Majeshi, Maafisa na Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa maafa makubwa yaliyowakuta na hasara waliyoipata kwa milipuko ya mabomu iliyotokea katika Ghala Kuu la Jeshi, Gongolamboto.

11. Baraza pia limelipongeza Jeshi kwa juhudi kubwa ilizofanya kuzima moto huo, hivyo kuweza kunusuru baadhi ya maghala, zana na vifaa vingine visiteketezwe na moto.

12. Baraza limeagiza Jeshi lifanye uchunguzi wake wa ndani wa chanzo cha tukio hili kama Sheria ya Ulinzi wa Taifa inavyoagiza. Aidha, imetaka vyombo vingine vya ulinzi na usalama visaidie katika uchunguzi huo.

13. Baraza la Usalama limeamua kuwa, Serikali ya Tanzania iombe nchi rafiki zisaidie katika uchunguzi wa chanzo cha tukio hili na kushauri namna bora zaidi ya kuimarisha usalama na uhifadhi wa mabomu na risasi katika maghala ya Jeshi letu kote nchini.

14. Mwisho, Baraza la Usalama wa Taifa linawaomba wananchi waliohama warejee kwenye makazo yao kwani kipindi cha hatari ya mabomu kulipuka kimekwishapita. Tunaomba na kusisitiza wajiepushe kuchezea mabomu yaliyodondoka katika maeneo yao ambayo bado hayajaondolewa.

Ndugu Wananchi Wenzangu;

Hili ni janga ambalo pamoja na kusikitisha linaleta uchungu hasa pale inapotokea miaka miwili tu baada ya janga la Mbagala. Machungu yenu ndiyo machungu yangu na ndiyo ya viongozi wote Wakuu wa Nchi yetu ambao ndiyo Wajumbe wa Baraza la Usalama la Taifa. Naomba tuwe watulivu katika wakati huu mgumu.

Napenda kuwahakikishia kuwa tumeamua kulishughulikia tatizo lenyewe na athari zake sasa na siku za usoni kwa uthabiti mkubwa. Naomba tuendelee kuwa na imani na Jeshi letu, viongozi wake na wanajeshi wetu wote. Tuwaunge mkono na kuwapa ushirikiano sasa na siku za usoni.

Mungu Ibariki Afrika!

Mungu Ibariki Tanzania!

Asanteni kwa kunisikiliza.

February 17, 2011

"Goms" si salama tena!

Wakati Makamu wa Rais Dr Ghalibu Bilali akioneshwa sehemu mabaki ya mabomu yaliyolipuka jana usiku, wakazi wa maeneo hayo wako kwenye pilika pilika za kuondoka maeneo hayo wakitafuta hifadhi popote watakapo pata, wengi wanaamini kuwa mabomu hayo uenda yakalipuka tena kama ilivyokuwa Mbagala hivyo ni heri nusu shari kuliko shari kamili.
Taarifa zimekuwa zikitolewa kuwa kuna watoto wengi wamepotea, wengi wako vituo vya polisi, uwanja wa Uhuru na Sabasaba, wito umetolewa waliopotelewa kwenda kuangalia ndugu na jamaa zao sehemu hizo.
Mpaka sasa idadi rasmi ya waliopoteza maisha kutokana na milipuko hiyo ya jana haijatolewa, inakisiwa kuwa wanaweza kufika mia moja, Waziri Mkuu amenukuliwa akisema ni zaidi ya ishirini na Mnadhimu Mkuu wa jeshi alinukuliwa na bbc kuwa ni 32, hakuna idadi rasmi mpaka sasa.
Tunawapa pole wale woote waliofikwa na majanga haya, waliojeruhiwa, waliofiwa na ndugu na jamaa zao pia, na zaidi tunawaombea heri marehemu wote, Mungu alaze roho za marehemu hao pema peponi. Amen.
Picha kwa hisani ya John Bukuku.

MABOMU GONGO LA MBOTO, Zaid ya 30 wanahofiwa kufa, mamia wajeruhiwa.

At least 32 people have been killed in multiple explosions after an accident at a munitions dump in Tanzania's commercial capital, Dar es Salaam, officials say.

The blasts lasted several hours at the Gongola Mboto military base.

The city's airport was reported to have been closed after the blasts, the British Foreign Office said.

Residents were encouraged to stay inside their homes and away from windows after the explosions.

Debris was hurled across the city and chief of staff Gen Abdurahman Shimbo said 32 people had died.

Earlier Prime Minister Mizengo Pinda said 17 bodies had been recovered.

Mr Pinda said the explosions had started in one depot before spreading to others in the camp.

By Thursday morning, 23 depots had been destroyed, along with two residential houses and a secondary school.

Mr Pinda told the National Assembly that at least 4,000 people were sheltering at the National Stadium, and warned the death toll could increase.

BBC

February 16, 2011

Watu kadhaa wahofiwa kufa katika milipuko kambi ya JWTZ Gongolamboto.

Kutoka hapa nilipo Kimara Suka naweza kuona miale mikubwa ya moto unaotokana na milipuko ya mabomu katika kambi ya JWTZ Gongolamboto ni kama yale yaliyotokea Mbagala mwaka juzi.
TAARIFA ZILIZOTUFIKIA NA AMBAZO HAZIJATHIBITISHWA TOKA ENEO LA TUKIO NI KUWA WATU KADHAA WANAOFIWA KUFA BAADA YA MOJA YA BOMU KUTUA KATIKA BASI LILILOKUWA NA ABIRIA AMBAO WALIKUWA WANAONDOKA MAENEO HAYO KUTAFUTA USALAMA ZAIDI BAADA YA KUANZA MILIPUKO USIKU HUU.

February 14, 2011

February 11, 2011

Da famous BONGA BAR.

Baa hii ilikuwa maarufu sana enzi zileeeeeee, wazee wa masanga wangapi wanaikumbuka?

February 1, 2011

10% to my target, THANK GOD

Hakika hakuna lilisilowezekana ukiamini, Bwana alisema omba lolote nami nitakupa, nimeomba mwaka huu unipe pato hili kwa mwezi na nimeona mkono wako. Asante Mungu.

Arts n' Photo sildes

"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION

Future Stars!

Some of published work

RIGHT TO BE RICH

RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576

Popular Posts

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...