January 30, 2008
Neno la wiki
Go Fish
I want to talk to you about the number one business of the Church: the business of winning souls. It is what I call “The Seven Cs of Soul Winning.
”The first “C”—commission—is found in Mark 16:15. These are some of the last words Jesus spoke before He ascended into heaven,
“Go into all the world and preach the gospel to every creature.”Could it be any clearer? Jesus said, “Go.” Dare we say, “No”? He said, “Go.”That is the opposite of “stay,” isn’t it? Go: G-O.God wants you and me to take the Gospel to Others.
You and I need to get out into the world! Jesus was not crucified between two candles on a church altar. He was crucified out in the byways and highways of humanity, and that is where we must take the message.Jesus said, “Follow Me, and I will make you become fishers of men.
” That is a promise. But you know what? You have to get to the water if you are going to catch fish. You have to get out of the four church walls, out to where hurting humanity is, and engage them with the gospel.A while back, I went backpacking with my two sons in a very remote area.
We found a pristine lake where just about every time we would put a line in the water, we would catch a fish.We also had this incredible camp. But you know what? If we wanted to catch fish, we had to go down to the water. No one could catch a fish sitting in camp.A lot of Christians just hang around the camp. They form fishing clubs and talk about how important it is to fish. But they don’t fish.
God wants us to go fish!
January 29, 2008
Marehemu Tumaini Mbaga
Yaaminika kuwa mwili uliokotwa uko Kwembe ukiwa umearibika vibaya kuwa ni wa aliyekuwa Dereva wa Naibu Waziri Usalama wa Raia aliyetoweka yapata wiki mbili sasa Bw Tumaini Mbaga,
pamoja na kuwa inasubiriwa taarifa ya mkemia mkuu, Mke wa dereva huyo ametambua baadhi ya vitu kama suruali, soksi na kitambaa kuwa ni vya mumewe,
Mpaka sasa hakuna aliyekamatwa kuhusishwa na utekaji au mauaji ya dereva huyo, na bado ni kitendawili kikubwa juu ya lengo hasa la wauaji wake hasa ikizingatiwa kuwa gari lilipatika likiwa limetelekezwa CCM Tabata siku moja tu baada ya kuchukuliwa CCM Temboni.
January 25, 2008
Driver wa Waziri yu Wapi?
Majaaliwa ya Driver wa Naibu Waziri Usalama wa Raia (POLICE) Tumaini Mbaga bado kujulikana karibia siku sita sasa toka kutoweka na gari katika mazingira ya kutatanisha huku Kimara Temboni na hatimaye Gari kupatikana likiwa limetelekezwa CCM Tabata,
Familia ya Driver huyo, baba wa watoto wenne watatu kike na kiume mmoja imebaki kuomba Mungu usiku na mchana ili apatikane kama si mzima basi hata mwili wake tu uonekane, hakika hiki ni kipindi kigumu sana kwa familia hii bila kujua nini kimeteokea kwa Mkuu wa familia.
Kwani kwa kupatikana kwa gari peke yake na ambalo yasemekana lilitelekezwa pale CCM Tabata siku moja tu baada ya kutoweka pasipo julikana wapi dereva alipo kiaacha uwezekano wa kumpata dereva huyo akiwa hai kuwa mdogo sana ni Muujiza wa MWENYEZI MUNGU TU unaoweza kufanya vinginevyo.
January 23, 2008
Mawasiliano.....
Fiber Optic.....
Ule mradi wa kupitisha waya wa mawasiliano chini ya bahari (Fiber optic Network) utafiti wake sasa umekamilika, Mkurugenzi wa Saecom Tanzania Michael Njumba asema mawasiliano yatakuwa rahisi kwa zaidi ya 50% kuliko sasa ya satelite. hii ni meli maarumu ya utafiti imekamisha kazi yake ya utafiti ya zaidi ya miezi 5.
Wapenzi wa soka kaeeni chonjo kwani baada ya kukamilika mradi huu hapo 2009 kombe la dunnia 2010 Bondeni hatutaitaji kulipia tena kila kitu ni bwelelele.
Wadau kwa Bongo ni Michael Njumba na Anna Kahama.
January 22, 2008
Mikukus..
wale wapenzi wa kujichana na hasa makuku sasa watayapata ktk muonekano bora zaidi toka Interchick.
Mwenyekiti wa bodi wa Interchick Kalokola Bwesha na naibu waziri wa mifugo Dr Mlingwa wakipata vikorombwezo vya vyuku toka Interchick
wengi na hasa wakazi wa maeneo ya mbezi beach, kunduchi, tegeta na vitongoji kadhaa vya dar bado wakumbuka yale makuku ya wakti uleeeeeeeee sasa yamekuja tenaaaa.
BODI RUUM..
Mambo ya kushangaa ni mengi sana bongo na hasa hapo PAITWAPO BOT uwezi amini kuwa pamoja na minara yote hii miwili na jengo la kati lakini bodi room ni kiduchu kiasi kupita mpaka msuguane migongo!!!
hivi hilo jengo lote ambalo naamini kuwa ni kubwa kuliko pengine jengo lolote bongo isipokuwa labda bunge ni la kazi gani hasa?
au hata wafagizi wana ofisi zilinganazo na flooor nzima?
JK ndani ya BK.
1.Wazee wa mji wa Bukoba wakimpa zawadi za jadi Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika viwanja vya Uhuru mjini humo jana.baadaye Rais Kikwete alihutubia mkutano wa hadhara.
2.Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga ngoma ya mtawala wa jadi aliyokabidhiwa na wazee wa mji wa Bukoba juzi katika viwanja vya Uhuru mjini hapo.
3.Umati wa mamia wa wakazi wa mji wa Bukoba wakimshangilia Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipokuwa akiwahutubia juzi.
4.Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mzee Paulo Kilaini mwenye umri wa miaka 80 katika kijiji cha Katoma nje kidogo ya mji wa Bukoba juzi.Mzee Paulo Kilanini ni Baba Mzazi wa Askofu Msaidizi Jimbo kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Method Kilaini.Rais Kikwete alikwenda kijijini hapo kukagua maendeleo ya Shule ya msingi Kilaini iliypjengwa na Askofu huyo katika kiwanja alichokitoa Babu yake.
Kwa wale msofahamu mila za BK
VAZI la kanzu na koti ni vazi la heshima kwa Wazee wa mkoa huu na mara kijana anapooa upewa upewa kanzu, mkuki na mundu hii kutambua kwamba kijana sasa kawa mtu mzima na anaweza kuongea na kukaa na wazee wa kijiji na kutoa mchango wake, kama ujaoa hata kama utakuwa na miaka mia we ni mtoto tu huwezi ongea mbele za wazee.
January 19, 2008
CHETIIIIIZ
Hivi wabongo wenzangu wangapi tuna vyeti vya kuzaliwa?
si tulio home hata nyie mlo ng'ambo wangapi mnavyo?
LEO hii huku Bagamoyo RITA wamezindua campaign ya kusajjili watoto wote wanaozaliwa ili kila mtu awe nacho kwani haki ya kila mtoto kuwa na cheti.
Wapowasemao kupata cheti cha kifo ni rahisi zaidi kuliko cha kuzaliwa mhh?
TWIGA STARS
Timu yetu ya taifa ya soka ya wanawake Twiga Stars imeanza kambi kwaajili ya maandalizi ya mechi yao dhidi ya Cameroon mwezi February.
Twiga stars wanaitaji mchango wenu wadau wa sports wa kila hali hili kuwawezesha kushinda mechi hii na pengine kuchukua uchamps,
shime wapenzi wote wa sports tuipe kila aina ya support timu yetu hii ili nani ajueaye yaweza kututoa kimasomaso,
kwa kutambua hilo blog hii itakuwa inaweletea maendeleo ya timu yetu hii kila siku na pia picha zake hazita wekwa lebo ili wana blogger wapenda soka watakuwa huru kuzitumia ktk blog zao hasa rafiki yangu haki ngowi ili wanaotembelea blog zenu wapaje ujumbe na wanaotaka kuchangia basi wawasiliane nami ili niwaeleze namna ya kuchangia kwa ajili ya timu yetu.
TIMU iko chini ya mtaalamu Charles Mkwasa akisaidiwa na Siwa kwa upande wa makipa.
January 18, 2008
FORODHANI KUKARABATIWA...
Wale wapenzi rojorojo, mishikaki ya ngombe mpaka samaki na pweza au mwengo, ngisi nk pale Forodhani wakae mkao wa kula kwani bustani ile almaarufu zenji sasa yaboreshwa kwa msaada wa Aga Khan kwa kipindi cha miezi kumi hivi,
ila kwa sasa rojo hizo zitakuwa zikipatikana Ngome Kongwe ndani.
January 16, 2008
Subscribe to:
Posts (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Nimekuta ubishi paala fulani tena kwa watu naweza sema ni waelewa kiasi fulani maana wameenda shule na wengine wako katika fani, ati ile ho...
-
Prof Aloysius Mwessa Hnonoli ni Mbongo wa kwanza kuwa Mkurugenzi wa Muhimbili na Mkuu wa Chuo kikuu cha Tiba. Mstaafu huyu jana alitu...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
Ukumbi huko nyuma ya Minara miwili ukiwa ni wa mviringo. Eneoe kubwa la chai na ukaguzi pamoja na usajili kwa waalikwa. Sehemu za waa...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
Dr H Mwakyembe akishushwa toka ktk ndege ya kukodi na kupelekwa moja kwa moja MOI kwa Matibabu zaidi, Dr Mwakyembe alipata ajali ya gari m...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...