May 27, 2008
CHEE NKAPA AZOZA
RAIS Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa amevunja ukimya kuhusu tetesi na tuhuma kwamba alikiuka misingi na kujikita katika biashara wakati akiwa madarakani kwa kusema madai hayo si ya kweli na kwamba wanaomtuhumu wana chuki dhidi yake.
Akihutubia mwishoni mwa wiki katika Kijiji alichozaliwa cha Lupaso, Wilaya ya Masasi, Mkapa alisema wanaomtuhumu wanamchukia kwa kutowapendelea wakati wa utawala wake. Katika hotuba yake hiyo aliyoitoa wakati wa kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya tiba kwa Kituo cha Afya kinachomilikiwa na Kanisa la Katoliki kijijini hapo, alisema; “Msisikilize uongo huo kwa sababu hauna msingi wowote isipokuwa ni chuki …hasa inayotokana na watu ambao walifikiri nitawapendelea … sikuwapendelea,” alisema Mkapa huku akishangiliwa na wanakijiji wenzake waliohudhuria makabidhiano hayo.
Alisema kuwa yeye si tajiri na kwamba tuhuma hizo ni za uongo na hivyo kuwataka wananchi kuzipuuza kwa kuwa hazina msingi wowote wala chembe ya ukweli. “Sina uwezo wa fedha ingawa najua mnasikia na kusoma mengi …naishi kwa pensheni yangu kutoka serikalini kutokana na kuwa kiongozi kwa miaka 10 ambayo hata Mzee Mwinyi anaishi hivyo maana sisi sote ni wastaafu. Huo (uvumi) ni uongo …uongo ….uongo ….uongo …uongo….uongo….uongo,” alisema Mkapa na kuongeza; “Mimi si tajiri, nimeomba msaada nimepewa…nimejinyima mimi na mke wangu ndiyo tukaweza kugharimia kusafirisha vifaa hivi kutoka Canada hadi Dar es Salaam, kutoka hapo hadi hapa vimesafirishwa na Serikali…..sikuwa na uwezo wa kununua vifaa kama hivi. Nitapata wapi fedha za kununua vifaa kama hivi,” alisema Mkapa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
It has been a while now that my life had taken on a sense of expectation. It has been almost 3 months since I met Russell Simmons at a char...
-
It’s not important to hold all the good cards in life. It`s important how well you play the cards which you hold. Often, when we lose...
-
Tanzania denies it’s slowing down integration in East Africa. APA-Kampala (Uganda) Members of the East African Legislative Assembly from...
-
LONDON (Dow Jones)--U.K. defense giant BAE Systems PLC (BA.LN) Tuesday was fined GBP500,000 for improper accounting in relation to the award...
-
On Tuesday, 7th July we witnessed the peak of the Saba Saba festivities. I never go to the Dar es Salaam International Trade Fair, these day...
-
Gadhafi na Obama With reported pockets of fighting remaining in Tripoli on Wednesday, the whereabouts of Lib...
-
The government of Uganda is planning to pay a compensation fee to the government of Tanzania for the help offered Uganda in the 1979 liber...
-
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wakurugenzi watendaji wa mitandao ya simu za mikononi za Zain, Zantel na Tigo. kutoka kushoto ni bwana N...
1 comment:
Ebwana unatudanganya katika hiyo picha yako ya hapo pembeni. hivi unaweza kweli kupiga picha hapo ilhali jicho la kushoto lipo wazi?
Nipe jibu.
Post a Comment