WAKATI Mjadala wa Dowans ukibaki kwenye swali la nani mmiliki wake, raia wa Oman, Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi amejitokeza na kukiri kuimiliki kampuni hiyo inayoidai Tanzania mabilioni ya shilingi. Al Adawi alikutana na wahariri wa vyombo vya habari nchini jana na kueleza ujio wake kuwa umelenga kukutana na Tanesco na kujadili suala la malipo ya Sh94 bilioni ambayo kampuni yake inaidai Tanzania.
Ujio wa Al Adawi umemaliza mjadala uliogubika umiliki wa Dowans na kuwachanganya Watanzania huku baadhi yao wakiamini kuwa kampuni hiyo inamilikiwa na mfanyabiashara maarufu nchini, Rostam Aziz. Al Adawi ni mmoja wa watu ambao majina yao yako kwa Wakala wa Usajili wa Kampuni nchini (Brela) waliojiandikisha kama wamiliki wa kampuni hiyo ya Dowans.
Watu wengine waliotajwa na Brela kuwa ni wamiliki wa Dowans Tanzania Ltd, ambao ni Dowans Holding S.A, Costa Rica na Portek Systems and Equipment (PTE) Ltd na uraia wao kwenye mabano ni Andrew James Tice na Guy Picard (Canada), Gopalakrishnan Balachandaran (India), Stanley Munai (Kenya) na Hon Sung Woo (Singapore).
Akizungumza katika mkutano huo huku akigoma kupigwa picha, Al Adawi alisema yuko tayari kuzungumza na Tanesco kuhusu fidia ya Sh94 bilioni (hakutaja kiasi), baada ya kuvunjwa kwa mkataba baina ya kampuni yake hiyo na Tanesco.
"Nimekuja kwa mambo mawili; moja ni kuondoa sintofahamu iliyopo hivi sasa kuhusu kampuni ya Dowans na kuangalia kama kuna uwezekano wa kuwapo suluhisho la kile kilichopo hivi sasa kuhusu Dowans," alisema Al Adawi. Kwa mujibu wa mfanyabiashara huyo, ambaye ni Mwanajeshi aliyestaafu katika ngazi ya Brigedia Jenerali, Tanzania ni nchi inayovutia kibiashara na inayofuata sheria za uwekezaji.
Source: Mwananchi
February 21, 2011
Mmiliki wa Dowans akataa kukutana na Ngeleja na kupigwa picha
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
It has been a while now that my life had taken on a sense of expectation. It has been almost 3 months since I met Russell Simmons at a char...
-
It’s not important to hold all the good cards in life. It`s important how well you play the cards which you hold. Often, when we lose...
-
Gadhafi na Obama With reported pockets of fighting remaining in Tripoli on Wednesday, the whereabouts of Lib...
-
MALUIMBANO kuhusu waraka wa Kanisa Katoliki (RC) yanaendelea kuwa makali, baada ya waumini wa kanisa hilo kumuelezea mwanasiasa mkongwe nchi...
-
Thank you. Thank you. Thank you so much. (Sustained cheers, applause.) Tonight, more than 200 years after a former colony w...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
-
Can You Make Money with FLP?—A Review of Forever Living Products Je ni kweli waweza ingiza kipato kwa kupitia biashara ya mtandao Forever? ...
-
Maharamia wa KISOMALI JUZI ALMANUSURA WAPORE MELI KTK PWANI YA DAR. Somali pirates fail to seize ship off Tanzania KUALA LUMPUR, Malaysia...
1 comment:
Great info! Thanks for sharing. ;)
Chris
Post a Comment