August 17, 2008
Brig General Nyambibo atunaye tena
JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
Agosti16, 2008
PRESS RELEASE
Mkuu wa Chuo cha Kijeshi (TMA), Monduli Arusha, Brigedia Jenerali January Nyambibo amefariki Dunia katika Hospitali Kuu ya Kijeshi Lugalo Agosti 15, 2008 kwa ugonjwa.
Mipango ya mazishi inafanywa na Makao Makuu ya Jeshi kwa kushirikiana na familia yake. Msiba uko nyumbani kwa kaka yake Luteni Kanali Mstaafu Jackton Nyambibo, Gongo la Mboto Ukonga jijini Dar es Salaam karibu na hospitali ya Mather Care.
Marehemu atazikwa kwa heshima zote za kijeshi Jumatatu, Agosti 18, 2008 saa kumi alasiri katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Wakati wa uhai wake, Brigedia Jenerali Nyambibo alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo, Msaidizi wa Mnadhimu Mkuu, Mkufunzi Mkuu TMA na Shule ya Mafunzo ya Infantria (SMI) Mgulani, Mwambata Jeshi nchini Msumbiji na Mkuu wa Chuo TMA wadhifa aliokuwa nao hadi alipofariki dunia.
Marehemu Nyambibo alizaliwa mkoani Mara mwaka 1953 na kupata elimu yake ya msingi na Sekondari mkoani Mara hadi mwaka 1971 alipojiunga na Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Wakati wa utumishi wake jeshini, marehemu alipandishwa vyeo katika ngazi mbalimbali na kupata cheo cha Brigedia Jenerali Agosti 30, 2006 cheo alichofariki nacho.
Brigedia Jenerali Nyambibo atakumbukwa kwa mchango wake alioutoa wakati wa ukombozi Kusini mwa Afrika pale alipokuwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha Mgagao mkoani Iringa kilichokuwa na jukumu la kuwafundisha wapigania uhuru wa Chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini.
Imetolewa na Kitengo cha Habari
Makao Makuu ya Jeshi
Upanga, Dar es Salaam
RIP.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
Kumbe tuna utalii wa aina nyingi sana Tanzania!! mpaka huu nao? Waliingizia taifa dola ngapi? Women seeking beach boys ...
-
It has been a while now that my life had taken on a sense of expectation. It has been almost 3 months since I met Russell Simmons at a char...
-
It’s not important to hold all the good cards in life. It`s important how well you play the cards which you hold. Often, when we lose...
-
Tanzania denies it’s slowing down integration in East Africa. APA-Kampala (Uganda) Members of the East African Legislative Assembly from...
-
LONDON (Dow Jones)--U.K. defense giant BAE Systems PLC (BA.LN) Tuesday was fined GBP500,000 for improper accounting in relation to the award...
-
Edmark International founder, Chief Executive Officer and Chairman. Edmark Tanzania welcomes all entrepreneurs, business people a...
-
On Tuesday, 7th July we witnessed the peak of the Saba Saba festivities. I never go to the Dar es Salaam International Trade Fair, these day...
-
Gadhafi na Obama With reported pockets of fighting remaining in Tripoli on Wednesday, the whereabouts of Lib...
-
Shibe inapoua kuliko njaa Obesity kills more people than hunger Most of the world's populations live in countries where overweight a...
No comments:
Post a Comment