Pages

July 31, 2007

What is 500 million? is just a peanut!! Aonekana kushangaa Wakili Maarufu, Mbunge na pia Mfanyabiashara Mkono wakti akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Benk M ambayo anasema ni ya kwake pamoja na wanahisa ambao hakuwataja, na kwamba haina uhusiano wowote na Rais Mstaafu Ben Mkapa, anadai kuwa kwa mtu wa rangi yake kuniliki ardhi katikati ya jiji ni ndoto, na kwamba ni ndoto pia kumiliki benki kwa mzawa kama yeye ndo maana ya makombora yanayorushwa kwake pitia magazeti fulani kwa lengo la kuhakikisha hafanikiwi. Kwa madai yake ni kwamba toka 1991 ametaka kuanzisha benki maarufu kama Shilingi House lakini haikuwezekana. Kama hayo yote ni kweli basi ni nani hao wanaorusiwa kumiliki ardhi katikati ya jiji? na wanamilikishwa na nani? na ni biashara gani mzawa katika nchi yake anapaswa kufanya? ni umachinga tu? na nani hasa hao wanaoweka vizingiti ivi na kwa faida au hasara ya nani? maswali ni mengi mno na sijui kama majibu yaweza patikana. Tatizo liko wapi hasa?

No comments:

Post a Comment