Pages

February 17, 2010

CHONDE CHONDE WATANI, THIS IS TOO MUCH!!

Habari zilizorushwa toka jana na leo ktk vyombo mbalimbali vya habari kuhusu mauaji ya kutisha ya familia tatu za ukoo mmoja kwa kuchinjwa kama kuku huko Mara zinasikitisha sana. Hivi mtu au watu na akili zao timamu wanawezaje kutenda unyama kama huo kuua watu 17 pamoja na watoto wanaonyonya katika nyumba tatu na tena bila kuonekana? Hii inasikitisha sana, kwamba Tanzania sasa imefika mahali watu twauana kama au pengine kuliko hata wanyama? Enyi watani zangu huko Mara ni nini kimewasibu? ni kisasi gani hicho cha kulipita kwa katoto kachanga kasicho jua chochote duniani humu? Malaika hawa na wazazi na ndugu zao wamewatenda kikubwa kipi kisichoweza kurekebishika mpaka kwa ukali wa upanga? Huu ni unyama mkubwa kabisa wa enzi zetu ambao twazani tumustaharabika kidogo kuliko vizazi vilivyotangulia, lakini sasa nadhani baadhi yetu na hasa watani zangu

No comments:

Post a Comment