May 27, 2008
CHEE NKAPA AZOZA
RAIS Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa amevunja ukimya kuhusu tetesi na tuhuma kwamba alikiuka misingi na kujikita katika biashara wakati akiwa madarakani kwa kusema madai hayo si ya kweli na kwamba wanaomtuhumu wana chuki dhidi yake.
Akihutubia mwishoni mwa wiki katika Kijiji alichozaliwa cha Lupaso, Wilaya ya Masasi, Mkapa alisema wanaomtuhumu wanamchukia kwa kutowapendelea wakati wa utawala wake. Katika hotuba yake hiyo aliyoitoa wakati wa kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya tiba kwa Kituo cha Afya kinachomilikiwa na Kanisa la Katoliki kijijini hapo, alisema; “Msisikilize uongo huo kwa sababu hauna msingi wowote isipokuwa ni chuki …hasa inayotokana na watu ambao walifikiri nitawapendelea … sikuwapendelea,” alisema Mkapa huku akishangiliwa na wanakijiji wenzake waliohudhuria makabidhiano hayo.
Alisema kuwa yeye si tajiri na kwamba tuhuma hizo ni za uongo na hivyo kuwataka wananchi kuzipuuza kwa kuwa hazina msingi wowote wala chembe ya ukweli. “Sina uwezo wa fedha ingawa najua mnasikia na kusoma mengi …naishi kwa pensheni yangu kutoka serikalini kutokana na kuwa kiongozi kwa miaka 10 ambayo hata Mzee Mwinyi anaishi hivyo maana sisi sote ni wastaafu. Huo (uvumi) ni uongo …uongo ….uongo ….uongo …uongo….uongo….uongo,” alisema Mkapa na kuongeza; “Mimi si tajiri, nimeomba msaada nimepewa…nimejinyima mimi na mke wangu ndiyo tukaweza kugharimia kusafirisha vifaa hivi kutoka Canada hadi Dar es Salaam, kutoka hapo hadi hapa vimesafirishwa na Serikali…..sikuwa na uwezo wa kununua vifaa kama hivi. Nitapata wapi fedha za kununua vifaa kama hivi,” alisema Mkapa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Arts n' Photo sildes
"SILENT VOICES" PHOTO EXHIBITION
Future Stars!
Some of published work
RIGHT TO BE RICH
The ownership of money and property comes as a result of doing things in a certain way, and those who do things in this certain way — whether on purpose or accidentally — get rich, while those who do not do things in this certain way — no matter how hard they work or how able they are — remain poor. WDW Do things in RIGHT way now, but how? Call: +255716927070/+255784475576
Popular Posts
-
Chakula chapikwa karibu kabisa na vyoo vilivyo kulia. KABLA YA KUINGIA CAFETERIA WAKUTANA NA VITUUZI MLANGONI. BAFUNI NAKO NI BALAA. NA H...
-
At least 32 people have been killed in multiple explosions after an accident at a munitions dump in Tanzania's commercial capital, Dar e...
-
WADAU NADHANI SI VIBAYA SIKU MOJA MOJA TUKAPANUA MAWAZO KIDOGO NDO NAMNA YA KUELIMISHANA KUPITIA NJIA HII. HIKI ni kijiji kipo hapa bo...
-
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni-Kinondoni leo imeamua mazishi ya mwili wa Marehemu Paulo Goliama aliyefariki wiki iliyopita yafany...
-
Skandali ya BOT yazidi kuchemka.... NITOKE VIPI?????? BOT SAGA, MEGHJI AJIVUA.......... Meghji: I was duped by governor Ballali -Minist...
-
Kina dada wengi hivi sasa imekuwa ni kawaida kwenye kila shughuri hasa za usiku kukuta wamevaa nguo fupi, wengi wanasema ni fashion...
-
Edmark International founder, Chief Executive Officer and Chairman. Edmark Tanzania welcomes all entrepreneurs, business people a...
-
Mgonjwa wa saratani akipata huduma Ocean Road Cancer Insititute (ORCI) asubuhi leo hii baada ya kununuliwa kwa vifaa vilivyokuwa vimeibwa y...

1 comment:
Ebwana unatudanganya katika hiyo picha yako ya hapo pembeni. hivi unaweza kweli kupiga picha hapo ilhali jicho la kushoto lipo wazi?
Nipe jibu.
Post a Comment