Pages

February 26, 2008

Ziara ya Rais yaahirishwa

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS UNITED REPUBLIC OF TANZANIA Telephone: 255-22-2114512, 2116898 Fax: 255-22-2113425 PRESIDENT¢S OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM. Tanzania. TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Ziara ya Rais wa Uturuki yaahirishwa Na mwandishi maalum, `Ziara ya Rais wa Uturuki, Mheshimiwa Abdullah Gul katika Tanzania, iliyokuwa ianze leo, imeahirishwa.. Rais Gul alitarajiwa kuwasili nchini leo, kwa ziara rasmi ya siku mbili kwa mwaliko wa Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Rais Gul alitarajiwa kuwasili nchini na kundi kubwa la wafanyabiashara wapatao 160 kutoka Uturuki. Wakati wa ziara yake, mbali na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Kikwete, Rais Gul pia alitarajiwa kuhutubia mkutano wa pamoja wa wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki. Tanzania na Uturuki pia zilitarajiwa kutia saini mkataba wa ushirikiano wa kiufundi, kisayansi na kiuchumi katika eneo la kilimo. Imetolewa Na Bw. Salvator Rweyemamu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais na Habari, Ikulu, DAR ES SALAAM. 26 Februari, 2008

No comments:

Post a Comment